Jumatatu, 3 Aprili 2017

TFDA YAWANUA WATALAAMU WAKE MKOANI NJOMBE

 AFISA AFYA MKOA WA NJOMBE MATHIAS GAMBISHI AKICHANGIA HOJA


 HAWA NI WASHIRIKI WA KUTOKA  HALMASHAURI ZA MKOA WA NJOMBE AMBAO NI WATALAAM WA AFYA,MAAFISA BIASHARA, MAAFISA KILIMO, ASKALI WA POLISI NA WADAU WENGINE WA TFDA





 MENEJA TFDA KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI BWANA Rodney   Alananga

 MUWAKILISHI WA MKURUGENZI MKUU WA TFDA DKT SIKUBWABO NGENDABANKA AKIZUNGUMZA NA WASHIRIKI WA SEMINA HIYO



 AKIHITIMISHA SEMINA HIYO YA SIKU MBILI KAIM MGANGA MKUU SAMSON SORO SASI
















NJOMBE

Watalaamu Wa Mamlaka Ya Chakula Na Dawa TFDA  Waliopo Kwenye Halmashauri  Wametakiwa Kujenga Tabia Ya Kutoa Taarifa Kila Mwezi Za Kazi Wanazofanya Za  Utafiti Na Ukaguzi wa Maduka  Katika Halmashauri  Za Mkoa Wa Njombe Ili Kutambua Mambo Muhimu Yanayotakiwa Kufanyiwa Kazi.

Rai Hiyo Imetolewa Na Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa Wa Njombe Dkt  Samson Soro Sasi Wakati Akifunga Mafunzo Ya Siku Mbili Kwa   Watalaamu  Mbalimbali  Wanaounda Kamati  Ya Mamlaka Ya Chakula Na Dawa Katika Halmashauri Mkoani Hapa.

Dkt Soro Sasi  Amesema Kuwa Kwa Kipindi Chote Kumekuwa Na Changamoto Ya Baadhi Ya Watalaamu  Mbalimbali Wa TFDA Kutoa Taarifa  Pindi Wanapokuwa Wamefanya Kazi Ya Ukaguzi Kwenye Halmashauri Zao  Licha Ya Kufanya Kazi  Ili Kuwawajibisha Watakaokiuka Utaratibu Huo.

Dkt  Soro Sasi Ametaka Washiriki Wa Mafunzo Hayo Yalioandaliwa Na Mamlaka Ya Chakula Na Dawa TFDA Kwa  Watalaamu Wake Wa Halmashauri Za Mkoa Wa Njombe  Kutumia  Kikamilifu Kama Walivyokumbushwa Kwenye  Mafunzo Hayo Ili Kutoa  Elimu Kwa  Wafanyabiashara  Na Wananchi Juu Ya Kutumia Vyakula  Vilivyopitwa Muda Wake  Wa Matumizi Ya Binadamu.

Akizungumza Mara Baada Ya Kuhitimishwa Kwa Mafunzo Hayo Meneja Wa Mamlaka Ya Chakula Na Dawa Kanda Ya Nyanda Za Juu Kusini Rodney   Alananga  Amesema Mafunzo Hayo Yatasaidia Watalaamu Hao Kufuatilia Majengo Ambayo Hayajasajiliwa, Na Kutoa Elimu Kwa Wananchi Huku Wananchi Nao Kuonesha Ushirikiano Kwa TFDA Ili Kutoa Huduma Bora Ya Chakula Na Dawa.

Nao Baadhi Ya Washiriki Wa Mafunzo Hayo Wameshukuru  Kwa Elimu Iliyotolewa Kwani Kuna Baadhi Ya Mambo Yanayohusu Uingizwaji Wa Bidhaa Zisizosajiliwa  Ambapo Sasa Watakwenda Kugundua Badhaa Bandia Na Zisizobandia Ili Wananchi Wapate Huduma Ya Chakula Kilicho Salama.

Katika Mafunzo Hayo Yaliotolewa Kwa Siku Mbili Yamewahusisha  Wakaguzi Wa Halmashauri Za Mkoa Wa Njombe Wakiwemo  Jeshi La Polisi,Maafisa Afya, Maafisa Biashara,Kilimo Na Mifugo, Wafamasia,Wanasheria, Wahasibu Na Waganga Wakuu Wa Halmashauri Za Wilaya.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni