Jumanne, 21 Oktoba 2014

BASI LA MWAFRIKA LAPATA AJALI MKOANI NJOMBE



Basi la Mwafrika lililopata ajali mbaya 
eneo la Kibena mkoani Njombe 



Na Michael Mapollu, Njombe


Basi la Kampuni ya Mwafrika jana lilipinduka na kujeruhi abiria 32 ambao wamelazwa katika hospitali ya Kibena iliyopo mkoani Njombe baada ya kulikwepa basi la Super Feo lisigongane uso kwa uso.

Basi hilo lililikuwa likitoka wilayani Makete kwenda Iringa, ambapo ajali hiyo ilitokea saa 4:30 asubuhi katika eneo la kiwanda cha chai cha Kibena km 20 kutoka stendi kuu ya mjini Njombe lililopokuwa limesimama kushusha abiria.


Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo waliozungumza walisema chanzo cha ajali hiyo kilitokana na dereva wa basi la Mwafrika kulikwepa basi la Super Feo lililokuwa likipishana na trekta la kiwanda cha Chai ambalo lilikuwa likitoka kubeba majani ya chai.

Habari zilizopatikana kwenye eneo la tukio la ajali hiyo zilidai dereva aliyekuwa akiendesha basi hilo alifahamika kwa jina la Furaha Sanga ambaye alikimbia mara baada ya ajali hiyo kutokea, na kwamba basi hilo lilikuwa na zaidi ya abiria 50.

Akizungumza ofisini kwake, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Kibena, Dk. Patrick Msigwa alithibitisha hospitali hiyo kupokea majeruhi hao, ambapo wanawake walikuwa 16 na mawaume ni 15.

Dk. Msigwa aliwataja majeruhi hao ambao kati yao wamepata majeraha madogo madogo na wengine wakiwa wamevunjika viungo kuwa ni Eva Mligilwa (37) kutoka Ilambibole, Monica Kyando (61) mkazi wa Ikonda, Adela Mligo (12) mkazi wa Luponde, Winfrida Sanga (21) mkazi wa Ikonda, Rose Makweta (48) mkazi wa Ikonda, Martha Ngalau (30) mkazi wa Ikonda, Beatrice Fute (42) mkazi wa Ilambilole, Imara Irima (60) mkazi wa Ikonda, Safina Chaula (23) mkazi wa Makete na Daniel Daniel (27) mkazi wa Ikonda.

Wengine ni Pendo Bernado (62) mkazi wa Ikonda, Prisca Sanga (20) mkazi wa Mang’oto, Anna Sanga (28) mkazi wa Igola, Maria Sanga (37) mkazi wa Bulongwa, Mwale Lumbilo kutoka Igilamelewa, Erica Mwihuta (31) kutoka Mafinga na Jane Chengula (49) kutoka Makngarawe.

Dk. Msigwa aliwataja majeruhi wengine waliopata ajali hiyo kuwa ni Ambwene Mbilinyi (15) mkazi wa Ikonda, Rajab Sanga (24) mkazi wa Mbeya, Jeremiah Njeri (62) mkazi wa Mafinga, Betwel Sanga (30) mkazi wa Mbeya, Beni Lyalimi (40) mkazi wa Mhaji, Aidan Sekreji (71) mkazi wa Masisiwe, Victory Lupala (39) mkazi wa Isimila, Benito Ziku (22) mkazi wa Iringa, Mlende Chengula (29) mkazi wa Iringa, John Njasi (60) mkazi wa Mafinga, Onesmo Mkiwa (32) mkazi wa Mafinga, Isaya Lukulumbika (28) mkazi wa Mbalali, Hongela Lauli (32) mkazi wa Iruyo, Linus Matofari (30) mkazi wa Makete, Benedict Sanga (47) mkazi wa Mang’oto.

Alisema katika ya majeruhi hao, Sekreji ndiye hali yake iko chini ya uangalizi wa madaktari kutokana na kuvunjika mkono.

Mmoja wa majeruhi wa ajali hiyo, Linus Matofari akizungumzia chanzo cha ajali hiyo, alisema imesababishwa na harakati za dereva wa basi la Mwafrika namba T726AGA kutaka kulikwepa basi la Super Feo, ambalo lilikuwa limejaribu kulipita trekta la kiwanda cha chai Kibena.

Abiria alisema dereva wa basi hilo alikuwa katika mwendo wa kawaida tangu walipotoka kwenye Stendi ya mabasi ya mjini Njombe kuelekea na safari mkoani Iringa.

Kufuatia ajali hiyo, Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe, Fulgence Ngonyani jana alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kueleza hakuna abiria yoyote aliyepoteza maisha. Kamanda Ngonyani alisema ajali hiyo ilitokea majira ya saa 4: 30 asubuhi na kwamba dereva Furaha Sanga amekamatwa na chanzo cha ajali bado kinachunguzwa.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni