Jumapili, 14 Juni 2015

KILELE CHA MAADHIMISHO YA KONGAMANO LA VIJANA WAKATOLIKI KITAIFA KILICHOFANYIKA MKOANI NJOMBE KATIKA PICHA


ASKOFU wa Jimbo la Kuu la Songea mkoani Ruvuma, Damian Dallu akizungumza wakati wa misa maalum ya maadhimisho ya kilele cha kongamano la vijana wakatoliki kitaifa mjini Njombe 





Vijana wakatoliki kutoka mkoani Iringa wakiwa katika maandamano

Na Mwandishi Wetu 

ASKOFU wa Jimbo la Kuu la Songea mkoani Ruvuma, Damian Dallu amesema vijana wengi wamekuwa wakikosa ajira na kubaki wakilalamika kutokana na wazee wengi kuendelea kung’ang’ania madaraka na kugoma kustaafu jambo ambalo linaendelea kusababisha chuki miongoni mwa vijana hao.

Akizungumza jana katika misa maalum ya kufunga kongamano la Vijana wakatoliki Tanzania (VIWAMA) lililofanyika mkoani hapa na kuwakutanisha vijana mbalimbali kutoka majimbo 32 kati ya 34 nchini askofu Dallu alisema wazee ndio wanatakiwa kutumia busara kwa kuanza kustaafu kwa hiari badala ya kusubiri kuondolewa kwa nguvu.


“ukitaka kufanya kazi fanya, usingojee kuheshimika leo, utaheshimika baadaye ukitoka, na hili nalisema kwa wale wanaopenda madaraka hawataki kutoka, inaumiza kabisa, ukichukua wengine pale watahama hawatakuwa na wewe uliyepita zamani, watakuona ni mwema,” alisema Dallu.

“…ukiwa paroko au padre unafanya kazi pale mahari usingoje pale wakuambie baba umefaulu sana, nakuambia ni kazi bure, acha waseme baadaye wakati haupo, na watakuwa wanalinganisha na aliyepo,” alisema.

Askofu Dulla alitumia muda huo kumzungumzia Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kwa kusema alielewa baada ya kufariki dunia kuwa yeye ni nani katika safari yake ya kuwa kiongozi nchini.

“MWalimu Nyerere ameeleweka alichofanya baada ya kufa kwa hiyo ndugu zangu msiogope kuondoka madarakani, mfurahi yale yote mishale inapowaingia mkitoka itatoka, yatabaki makovu,” alisema.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni