Jumamosi, 17 Desemba 2016

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO DKT. ASHATU KIJAJI AHIMIZA MAENDELEO VIJIJINI


Mkuu wa mradi wa Agra, ambaye pia ni Mhadhiri katika Chuo Cha Mipango ya Maendeleo Vijijini-Dodoma, Dkt. Mark Msaki (kushoto), akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (Katikati) wakati akikagua maonesho ya taaluma, huduma na bidhaa kabla ya kutunuku tuzo mbalimbali kwa wahitimu 829 katika Mahafali ya 30 ya Chuo Cha Mipango ya Maendeleo Vijijini, Kituo cha Mwanza. Kushoto kwa Dkt. Kijaji na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula (Mb).


Mwanafunzi wa kiume wa Stashahada Mwaka wa Pili wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini, Kituo cha Mwanza, akielezea kuhusu mafunzo wanayoyapata chuoni hapo na namna elimu hiyo inavyosaidia kuendeleza vijiji walivyokwenda kufanya mazoezi kwa vitendo mkoani Mwanza, wakati Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (Hayupo pichani) alipotembelea na kukagua maonesho hayo ya taaluma, huduma na bidhaa zinazotolewa na chuo hicho.


Mwanafunzi wa kike wa Stashahada Mwaka wa Pili wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini, Kituo cha Mwanza, akielezea kuhusu mafunzo wanayoyapata chuoni hapo na namna elimu hiyo inavyosaidia kuendeleza vijiji walivyokwenda kufanya mazoezi kwa vitendo mkoani Mwanza, wakati Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (kushoto) alipotembelea na kukagua maonesho hayo ya taaluma, huduma na bidhaa zinazotolewa na chuo hicho.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (kushoto), akionesha moja ya machapisho yaliyotolewa na Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini wakati alipotembelea na kukagua maonesho ya taaluma, huduma na bidhaa kabla ya kutunuku tuzo mbalimbali kwa wahitimu 829 katika Mahafali ya 30 ya Chuo Cha Mipango ya Maendeleo Vijijini, Kituo cha Mwanza. 
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (kushoto), akisikiliza kwa makini maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Mkufunzi wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Bw. Ezekiel Kanire, (aliyeshika kipaza sauti) wakati alipotembelea na kukagua maonesho ya taaluma, huduma na bidhaa kabla ya kutunuku tuzo mbalimbali kwa wahitimu 829 katika Mahafali ya 30 ya Chuo Cha Mipango ya Maendeleo Vijijini, Kituo cha Mwanza. Kushoto kwa Dkt. Kijaji na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula (Mb).

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni