Alhamisi, 12 Machi 2015

WANAHABARI KUTOKA KIGOMA PRESS CLUB (KGPC) WATEMBELEA SHIRIKA LA DARAJA


Mkurugenzi wa Shirika la Daraja Development Ltd, Simon Mkina akizungumza na kuwakaribisha waandishi wa habari kutoka Kigoma Press Club (KGPC) walipotembelea ofisi za shirika hilo ambalo ni wachapishaji wa gazeti la Daraja Letu lenye makao yake mjini Njombe.



Mwenyekiti wa Kigoma Press Club, Deogratius Nsokolo akizungumza wakati walipotembelea ofisi za Shirika la Daraja Development Ltd kwa ajili ya kubadilishana uzoefu.


Na Mwandishi Wetu, Njombe

Timu ya Waandishi wa Habari kutoka Chama Cha Waandishi wa Habari mkoani Kigoma (KGPC) imefanya ziara siku tatu katika Shirika la Daraja Development Ltd ambao ni wachapishaji wa Gazeti la Daraja Letu lenye makao yake makuu mkoani Njombe, huku lengo kuu likiwa ni kubadilishana uzoefu wa kazi katika nyanja ya habari na masoko.

Katika ziara hiyo, viongozi wa KGPC walioko katika mafunzo hayo ni Mwenyekiti wa KGPC, Deogratius Nsokolo, Jacob Ezekiel Ruvilo ambaye ni Mhariri wa Gazeti la Kigoma Yetu, Fadhil Abdallah (Afisa Masoko wa gazeti la Kigoma Yetu na Katibu Mkuu Msaidizi wa KGPC), Emmanuel Matinde (Mhariri wa Michezo gazeti la Kigoma Yetu) na Mwajabu Hoza (Mweka Hazina Kigoma Yetu).

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni