Jumatatu, 23 Machi 2015

DK.SLAA KUBURUZWA KORTINI


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEienz1F6TaiRZjpnm4hHQHdv3kl3F0_Hlp7dAYzr1zDY9x2O4da7u25-r9F-ReJc-nt0pVJ1YIeeslTpFZy7XuRTi04tFrm5AbduUY7w8kkgM89obw-0as4fB8X-metEpXUVkFKEmd44gS1/s1600/3.jpg


NA KAROLI VINSENT

JESHI la Polsi Kanda Maalum ya Dar es Salaam lipo katika hatua ya mwisho katika kukamilisha ushahidi ili kumfikikisha mahakamani Katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema Dokta Wilbroad Slaa pamoja na  makada wa Chama  hicho.

Akizungumza na waandishi wa Habari mda huu Jijini Dar es Salaam Kamishna wa Polisi Kanda maalum Dar es Salaam Suleimani Kova ametaja sababu ya kumfikisha mahakamani katibu huyo wa Chadema na Makada wake inatokana na Vitendo vinavyodaiwa ni vya kinyama alivyofanyiwa mlinzi wake vya kumteka,kumpiga na kumlazimisha kutaja watu wanaomtuma kumuua Katibu mkuu wa Chadema.

Hivyo hivyo Jeshi hilo la Polisi limesema kwa sasa linawashikilia makada watatu wa Chama hicho kikuu cha upinzani nchini ambao ni Boniface Jacob miaka 32 mkazi wa ubungo kisiwani ambae pia ni diwani wa kata ya Ubungo kupitia chama hicho.

Sambamba na Hemed Ally Sabula miaka 48 mkazi wa Tandale kwa tumbo ambaye anadaiwa ni Afisa Usalama wa chama hicho Taifa.

Mbali na hao pia Kamishna Kova amemtaja Kada mwengine anayeshikiliwa kuwa ni Benson Mramba,miaka 30,mkazi Tabata Kisukulu ambaye ni Afisa Utawala wa Chadema.
Kamishna kova amebainisha kuwa Ushahidi wao utakapokamilika mafaili yao yatafikishwa kwa Wakili  wa Serikali ili hatua zichukuliwe.  

Aidha, Akizungumzia sakata la Mlinzi Kagenzi amesema kwa sasa wanamalizia kazi ya kukusanya ushahidi kutoka Chadema ambao wanamtuhumu bwana Kagenzi ambaye anafanya ushirikiano na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM bara Philip Mangula na Afisa Usalama wa Taifa Mkoa wa Kinondoni kwa kuaandaa mpango wa kutaka kumuwekea sumu Dokta Slaa.

Kesi hiyo kwa mala ya kwanza ilifika polisi tarehe 8 mwezi huu majira ya saa 11.jioni katika kituo cha Polisi cha Oysterbay kupitia kwa wakili wa Chadema anayetambulika kwa jina la john Malya akiambana na mtuhumiwa Khalid Kagenzi ambaye ni mkazi wa Tandale kwa tumbo ambapo Wakili huyo aliiambia polisi kwamba alimleta mtuhumiwa baada ya kuagizwa na Dokta Slaa ili kutoa malalamiko kwa niaba yake.

Ambapo Katika maelezo yake anadai Wakili huyo kuwa  uongozi wa Chadema ulikuwa ulichukuwa hatua mbalimbali dhidi ya kugenzi ikiwemo kumbana na kujilidhisha kuwa nahusika na mipango ya kimauaji.

Kwa mujibu wa Kamishna kova anasema katika mahojiano wakabaini kunavitendo vya kinyama ambavyo mlinzi huyo wa Dokta Slaa amefanyiwa na Makada wa Chadema baada ya Jeshi hilo kumkuta akiwa na majeraha mbalimbali katika mwili wake.

chanzo;full  habari

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni