Jumanne, 7 Oktoba 2014

WANYARWANDA KUCHEZESHA MECHI YA STARS NA BENIN JUMAPILI


Kikosi cha Taifa Stars kitakachokuwa na mabadiliko mengi

Na Mwandishi Wetu

MWAMUZI wa FIFA, Hakizimana Louis kutoka Rwanda ndiye atakayepuliza filimbi katika mechi baina ya Taifa Stars na Benin itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumapili, Oktoba 12, mwaka huu.

Hakizimana atasaidiwa na Wanyarwanda wenzake Simba Honore na Niyitegeka Jean Bosco.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), mechi hiyo itaanza kuchezwa saa 11 jioni.

"Mechi hiyo itatanguliwa na ile ya viongozi wa dini - Waislamu vs Wakristo kudumumisha upendo, amani na ushirikiano itakayoanza saa 9 kamili alasiri. Tiketi za elektroniki zitakazotumika kwa mechi hiyo tayari zimeanza kuuzwa kwa kiingilio cha Sh. 4,000 na Sh. 10,000," imesema taarifa hiyo iliyotolewa muda mfupi uliopita.

Wakati huo huo, Kocha wa Stars, Mart Nooij, ameongeza wachezaji watatu kwenye kikosi cha Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ili kukiongezea nguvu kwa ajili ya mechi hiyo. 


Wachezaji walioongezwa ni Jonas Mkude na Joram Mgeveke kutoka timu ya Simba, na Gadiel Michael wa Azam.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni