Jumanne, 7 Oktoba 2014

NGORONGORO YATOA NG'OMBE 20 ZENYE THAMANI YA MILIONI 20 KWA WANACHI WA WILAYA YA KARATU



Na Mwandishi Wetu

Ngorongoro: Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro(NCAA)imefanikiwa kutoa ng'ombe 20 wa kisasa wenye thamani ya zaidi ya milioni 20 kwa vijiji vinne vya Wilaya ya Karatu kwa madhumuni ya kuendeleza Uhifadhi wa maliasili ndani ya Vijiji hivyo.

Akiongea na waandishi wa habari mapema wiki hii Afisa Ugani wa Mamlaka hiyo ambaye ni Bw Salustin Hallu alisema kuwa huo ni moja ya miradi inayotekelezwa na mamlaka hiyo.


Alisema kuwa mradi huo ambao hapo awali ulianza rasmi na ng'ombe wa kisasa 20 uliweza kuwa na manufaa makubwa sana kwa Vijiji vya Troma, Ayalabe, lositete na Upperutele ambapo hapo awali baadhi ya wafugaji kwenye vijiji hivyo walikuwa wanalazimika kuchunga ndani ya hifadhi

Alifaafanua kuwa mpaka sasa zaidi ya familia 98 kwenye mradi huo tayari wameshanufaika kwa kuwa kila familia moja sasa ina ng'ombe wa kisasa mmoja na lengo halisi likiwa ni kuhakikisha kuwa kila familia inajijengea uwezo wa kuchunga ndani na wala sio kutoa mifugo kwenda kutafuta malisho nje.

“Ngorongoro inalinda sana ujirani mwema na wananchi wake na ndio maana tukaona kuwa badala ya kuwakataza tu wananchi wasiingie kwenye pori ambapo ni hatari kwa maisha yao wao pamoja na mifugo lakini pia tuwape mbinu mbadala za kuhakikisha kuwa wanajikomboa ndio maana tukaanzisha huu mpango ambao umeonekana kuwasaida sana wananchi wa hivi vijiji,” aliongeza Hallu.

Awali alisema Mamlaka pia bado ina mkakati mbalimbali wa kuhakikisha kuwa wanaweza kufikia familia zote sanjari na kuwapa elimu mbalimbali juu ya umuhimu wa kufuga ndani laki ni pia kuwapa mbinu imara ambazo zinatakiwa kutumiwa na wafugaji wa kisasa zaidi.

Akiongea kwa niaba ya familia 98 ambazo zimenufaika na mradi huo wa ngombe wa kisasa kutoka Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro bi Emirita Martin alidai kuwa pamoja na kuwa wamepata ng'ombe lakini bado Mradi huo unapaswa kuongezewa ngombe ambao wataweza kuwanufaisha wanawake.

Bi Emirita alibainisha kuwa kama kila Boma na familia zitapata ng'ombe mmoja ambaye atazaliana basi wakina mama wataondokana na dhana ya kuwa tegemezi kwenye maisha ya kifamilia kwani ufugaji unabadilisha maisha duni na maskini ambayo wanayo baadhi ya wanawake katika Wilaya hiyo ya Karatu.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni