Jumatatu, 20 Oktoba 2014

BREAKNEWZZ!!! Ndanda FC yamtimua Kocha

Wakati michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara ikizidi kushika kasi,timu ya Ndanda FC ya mjini Mtwara imemfukuza kocha wa timu hiyo Dennis Kitambi pamoja na kocha wa Magoli kipa Mohamed Mwarami.




Akizungumza na Kituo cha redio cha East Africa, Seleman Kachele amesema wamefikia hatua hiyo baada ya uongozi kukaa kikao cha dharura na kujadili mambo mbalimbali yaliyopelekea timu hiyo kufungwa katika mechi zake za Ligi Kuu hivyo wakaamua kuchukua uamuzi huo.

Kachele amesema, timu hiyo itakuwa chini ya mkurugenzi wa Ufundi Mahibu Kanu mpaka pale watakapopata kocha wa kuchukua mikoba ya Kitambi na Mwarami.


Kufuatia kutimuliwa kwa kocha huyo, pia Klabu ya Ndanda FC imetangaza nafasi ya Katibu Mkuu wa klabu hiyo ambaye ataiongoza klabu hiyo. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni