Alhamisi, 4 Septemba 2014

NJOREFA WAKABIDHIWA VIFAA VYA UJENZI WA OFISI YA CHAMA CHA SOKA


Makabidhiano ya bati yaliyofanyika nje zinapojengwa ofisi za chama cha mpira  Mkoa wa Njombe ( Njolefa) kutoka kushoto ni  Mkurugenzi wa shirika la Tanwat Rajeev Singh, Edymund  Munubi afisa tawala wa Tanwat, Katibu wa Chama cha Mpira Mkoa wa Njombe  Steven Njowoka na wa Mwisho ni Afisa Utamaduni na michezo Mkoa wa Njombe Steven Sanga. Picha na James Festo.

 Waandishi wa habari kazini
 Mkurugenzi wa kampuni ya Tanwat, Rajeev Singh akisalimiana Macho.
 Ni mfano wa mbao 77 ambazo zilitolewa na Mmiliki wa shule ya Hagafilo Bw Edward Mwalongo wa kwanza kushoto.
 Diwani wa kata ya Uwemba Bw Edward Mwalongo (kutoka kushoto) wa pili ni Katibu wa chama Mkoa Bw Njowoka , Raymond Ngondola   mkurugenzi wa shirika la Jr fire familigation na mwisho ni Afisa utamaduni  Mkoa Bw Sanga.
 

Na Mwandishi Wetu, Njombe.

CHAMA  chama cha mpira  Mkoa wa Njombe kimepokea mchango  wa bati, saruji na mbao wenye thamani ya zaidi ya  shilingi milioni  moja kutoka kwa wadau wa michezo zitakazazosaidia kuendelea kujenga ofisi zao ngazi za mkoa. Akiongea katika makabidhiano katibu wa chama hicho  Steven Njowoka alisema kuwa wamepokea   michango kutoka kwa wadau  ambapo hapo juzi walifanikiwa kupokea bati 53, Mifuko ya saruji  kumi na mbao  77 vyote vyenye thamani ya shilingi milioni  1,295,000/= na kufanya jumla ya michango kutoka kwa wadau wa michezo kufikia shilingi  milioni  1,891,000/=. Njowoka aliendelea kuwaomba wadau mbalimbali ndani na nje ya mkoa wa Njombe kuendelea kuchangia mchango utakaokifanya chama hicho mkoa wa Njombe kukamiliisha ujenzi wa ofisi zenye vyumba saba vilivyofikia hatua ya kupauliwa  kwani hivi sasa wanafanya kazi katika jengo ambalo wamepangishwa.

"sisi kama chama cha mpira bado tunahitaji kusaidiwa ...lengo letu ni kuwa hosteri yenye uwezo wa kulaza wachezaji na unapotaka  kuchangia usiangalie sura ya Njowoka angalia Njorefa inafa inahitaji nini kutoka kwako"alisema Katibu wa Njorefa. Katibu huyo aliwataja wadau wakubwa  waliotoa michango hiyo kuwa ni pamoja na Mkurugenzi wa shirika la Tanwat  Rajeev Singh ambaye  alitoa Bati zenye thamani ya shilingi laki nane, Diwani wa kata ya Uwemba Bw. Edward  Mwalongo ambaye alichangia mbao zenye thamani ya shilingi 355000/= na Mkurugenzi wa kampuni ya Jr fire familigaion  Bw Raymond Ngondola alitoa mifuko  kumi ya saruji yenye thamani ya shilingi 140,000/=.

 Naye Afisa Utamaduni na michezo Mkoa wa Njombe Steven Sanga alitumia fursa hiyo kuwakumbusha viongozi wa timu mbalimbali kuhakikisha wanaweka mipango madhubuti itakayoifanya michezo kusonga mbele  ikiwa pamoja na  kufuata taratibu na kubainisha kuwa viwanja vingi vya michezo Mkoani hapa  vinamilikiwa na taasisi za elimu hali ambayo inawalazimu kuanza kufanya marekebisho ili kuvitumia katika michezo.
  Nao baadhi ya wadau hao, Rajeev Singh na Raymond Ngongola aliwasihi  wazazi kuachana na itikadi ya kudhani michezo ni uhuni badala yake kuanza kufikiria kuwa michezo huchangamsha akili ya mwanafunzi na kuahidi kuendelea kukichangia chama hicho.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni