Ijumaa, 8 Agosti 2014

DROGBA ASTAAFU SOKA YA KIMATAIFA

Drogba alisaidia nchi yake katika upatanishi baada ya mgogoro wa kisiasa

Mchezaji soka maarufu wa Ivory Coast Didier Drogba, ametangaza kustaafu kutoka katika soka ya kimataifa.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 36, alichezea Ivory Coast zaidi ya mara miamoja.
Alishiriki kombe la dunia mara tatu na mashindano ya kombe la Afrika mara 2
Amesema kuwa anajivunia kusaidia nchi yake kufika katika nafasi hiyo kimataifa.

Drogba alipigia debe kumalizika kwa mgogoro wa kisiasa na pia kuhimiza pande zilizozozana kupatana.
BBC/SWAHILI
P


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni