Jumatatu, 21 Mei 2018

AKAMATWA KWA KUJIITA YEYE NI IGP SIMON SIRRO


Maricha Mniko (30) ambaye ni mtuhumiwa aliyekamatwa na Jeshi la Polisi Mkoani Njombe baada ya kufanya utapeli wa kujitambulisha yeye ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro akiwa mbele ya Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Njombe, Renata Mzinga alipozungumza  na Waandishi wa Habari mjini Njombe.

JESHI la Polisi Mkoani Njombe linamshikilia mkazi wa Tandala, Wilayani Makete Maricha Mniko (30) ambaye kabila ni Mkurya na kazi yake ni dereva kwa tuhuma za kutaka kufanya utapeli kwa kujiita yeye ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro na anahitaji kupata msaada wa gari ili alitumie kwa ajili ya kwenda nalo mkoani Mara.

Akizungumza kutoka ofisini kwake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Renata Mzinga alisema kuwa mnamo Mei 18, mwaka huu majira ya saa nne asubuhi mmiliki wa kampuni ya mabasi ya Japanes ya mkoani Njombe, Daniel Hatanaka alipigiwa simu na mwananchi huyo akijitambulisha kuwa yeye ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Simon Sirro.

"Akimweleza kuwa ana matatizo ya kijana wake ambaye anakesi huko Mara, hivyo anahitaji ampatie gari kwa ajili ya kufanya shughuli zake," alisema Renata.

Kamanda huyo alisema baada ya mmiliki huyo kupigiwa simu hiyo, aliweza kumhoji tapeli huyo kujua namba yake ameipata wapi, lakini kwa mujibu wa maelezo ya mtuhumiwa huyo alimweleza kuwa namba ya mmiliki huyo aliipata kupitia kwa Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Njombe.

"Hivyo mmiliki huyo aliamua kuwasiliana na sisi jeshi la polisi na sisi kwa kutupa hiyo namba kwa kuwa tunazitambua hizo namba za mkuu wa jeshi la polisi, tuliona moja kwa moja kuwa siyo namba za mmiliki mkuu wa jeshi la polisi," alisema Renata.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni