Jumamosi, 17 Desemba 2016

WAZIRI MKUU MAJALIWA AENDELEA NA ZIARA HALMASHAURI YA ARUSHA,AHUTUBIA MKUTANO WA HADHARA NAMANGA NA KUKABIDHI PIKIPIKI KWA VIJANA WA BODABODA

 Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akimtwisha ndoo ya maji bibi Agness Silima ikiwa ni ishara ya kuzindua mradi wa maji wa kijiji cha Onderet wilayani Arusha 
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akipiga ngoma ya msanja iliyokuwa ikichezwa na wnanwake wa Arusha baada ya kuwasili kwenye kijiji cha Ondenderet wilayani Arusha Desemba 27, 2016.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama ngoma ya wanawake wa kimasai baada ya kuzindua mradi wa maji wa kijiji cha Ondenderet wilayani Arusha Desemba 27, 2016. kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo.


 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikabidhiwa kirungu na wazee wa kimasai ikiwa ni ishara ya kumsimika kuwa mmoja wa wazee wa kabila hilo katika mkutano wa hadhara aliouhutubia katika kijjiji cha Namanga kilichopo kwenye mpaka wa Kenya na Tanzania  wilayani Longido
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wazee wa kimasai baada ya kuhutubia mkutano wa hadhara katika kijiji cha Namanga kilichopo kwenye mpaka wa Kenya na Tanzania wilayani Longido Desemba 16, 2016.  Wapili kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Desemba 16, 2016 alikabidhi pikipiki 10 kwa vijana wa bodaboda wa Namanga na  Longido  mkoani Arusha . Pichani, Waziri Mkuu akikabidhi pikipiki hizo baada ya kuhutubia mkuano wa hadhara katika kijiji hicho.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni