Jumamosi, 17 Desemba 2016

Ushindi mwingine wa Yanga dhidi ya JKT Ruvu leo uwanja wa Uhuru


Ligi Kuu soka Tanzania bara mzunguuko wa pili ulianza leo December 17 kwa michezo kadhaa kuchezwa, kwa Mabingwa wa tetezi wa Ligi timu ya Yanga walianza kwa kucheza dhidi ya JKT Ruvu katika uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.
Yanga ambao walikuwa kama wageni dhidi ya JKT Ruvu wameibuka na ushindi wa goli 3-0, magoli ya Yanga yakifungwa na Simon Msuva aliyefunga magoli mawili katika ushindi huo na kusababisha goli la kwanza ambalo Michael Aidan alijifunga.
Ushindi huo unaifanya Yanga kuwa wababe wa JKT Ruvu, kwani katika mchezo wa mzunguko wa kwanza uliyochezwa October 26 2016 katika uwanja wa Uhuru waliwafunga tena kwa jumla ya magoli 4-0, magoli yakifungwa na  Obrey Chirwa dakika ya 6, Amissi Tambwe dakika ya 64, 92 na Simon Msuva dakika ya 83
.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni