Jumanne, 5 Mei 2015

Picha 8 za Mwenyekiti wa ‪ CHADEMA‬ Freeman Mbowe Alivyoungana na DC wa Kinondoni Paul Makonda Kutatua Mgomo wa Mabasi leo Ubungo Dar es salaam

Mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA mh Freeman Mbowe aliwasili leo katika stend ya mabas ubungo kuzungumza na madereva ambao walikuwa wakiendelea na mgomo na kuitaka serikali iwasikilize shida zao.
  
Mbowe ambaye aliwasili  majira ya saa nne kasoroo asubuhi alijikuta katika wakati mgumu baada ya wananchi kumshangilia kwa nguvu huku wengine wakifuta barabara ili gari yake ipite huku nyimbo za Ukawa zikiimbwa,jambo ambalo lilizua taharuki katika eneo hilo.

Kuhusu mgomo huo mkuu wa wilaya ya Kinondoni mh PAUL MAKONDA aliwaomba madereva hao kuendelea na kazi na ndani ya siku saba serikali itakua tayari imeshatoa tamko.

Madereva hao wamekubali kuanza safari kwa sharti la ndani ya siku saba wawe wamesikilizwa kero zao.








Hakuna maoni:

Chapisha Maoni