Jumatano, 13 Mei 2015

BAMAGA -AFRIKA SANA SINZA TAABAN KWA MAFURIKO.!

Pichani ni sehemu ya barabara kutoka Bamaga kuelekea Afrikasana Sinza jijini Dar ikiwa hoi bin taaaban baada ya kufunikwa na maji kufuatia mvua ambazo zimekuwa zikiendelea kunyesha jijini,aidha mafuriko hayo yamekuwa yakisababishwa pia na mitalo mingi ya eneo hilo kuzibwa na takataka zinazotupwa holela,matokeo yake maji yamekuwa yakikosa muelekeo.Idara husika wanapaswa kulifanyia kazi ipasavyo eneo hilo kwani limekuwa ni kero kubwa kwa wanaotumia barabara hiyo kila wakati kwenda kwenye shughuli zao za kila siku.
 Hali halisi ndio hivi mvua ikinyesha jijini Dar,kwa eneo la Bamaga.
Maji yakiwa yametuama tuliiii eneo la bamaga kuelekea Afrikasana

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni