Alhamisi, 8 Januari 2015

YANGA YAMTEMA JUMA KASEJA.

Uongozi wa klabu ya Yanga imetuma majina 23 kwa ajili ya kikosi chao kitakachoshiriki michuano ya Kombe la Shirikisho lakini imemtema kipa Juma Kaseja.

Katika majina majina yaliyotumwa kwenye makao makuu ya Shirikisho la Soka Afrika (Caf), hakuna jina la Kaseja.

Caf imeipanga Yanga kuanza na BDF ya Botswana ambayo ni timu inayomilikiwa na jeshi la ulinzi la nchi hiyo.
Habari za uhakika kutoka Caf zimesema, Yanga haijatuma jina la Kaseja na kusisitiza “hayumo”.
“Nimeangalia, hakuna jina la Kaseja. Je, una swali jingine,” alihoji ofisa huyo wa Caf.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni