Jumatatu, 12 Januari 2015

MBUNGE JOSEPH MBILINYI "SUGU" APATA AJALI YA GARI MLIMA KITONGA, ANGALIA PICHA ZOTE HAPA

IMG-20150110-WA0041

Kuna taarifa zilizoenea jioni ya January 10 kupitia mitandao mbalimbali, watu wametumiana picha na taarifa kwamba Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi amepata ajali.

Picha zilizoenea zinaonyesha Mbunge huyo amesimama na watu kadhaa pembeni ya gari aina ya Land Cruiser iliyopinduka.

Taarifa ya uhakika niliyoipata kuhusu tukio hilo ni kwamba Mbunge huyo amepata ajali akiwa na wenzake wanne ndani ya gari wakitoka Mbeya kuelekea Dar, ajali hiyo imetokea eneo la Kitonga, Iringa eneo ambalo lina kona kali za barabara.
Taarifa iliyoandikwa na mwandishi Francis Godwin kwenye matukiodaima.co.tz imesema hakuna mtu aliyefariki wala kupata majeraha makubwa ila Mbunge huyo ana michubuko midogo midogo, Kamanda wa Polisi Iringa, Ramadhani Mungi amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

IMG-20150110-WA0039
IMG-20150110-WA0040 (1)
IMG-20150110-WA0040
IMG-20150110-WA0041
IMG-20150110-WA0021
IMG-20150110-WA0023
IMG-20150110-WA0025
IMG-20150110-WA0027

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni