Jumatatu, 20 Oktoba 2014

NHC YATUMIA SHILINGI 731,360,000 KUSAIDIA MIRADI YA VIJANA


Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limetumia jumla ya shilingi milioni 731,360,000/= kusaidia miradi ya vijana ya kufyatua tofali nchini.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Kitengo cha Huduma na Mawasiliano wa NHC, Bi Suzan Omari wakati wa Kikao kazi cha Maafisa Vijana kilichofanyika hivi karibuni mkoani Tabora.
Bibi Suzan amefafanua kuwa fedha hizo  zinahusisha ununuzi wa mashine uliyogharimu shilingi 297,000,000/=, mafunzo ya wakufunzi yaliyogharimu shilingi 47,000,000/= na  uwezeshaji mtaji wa kuanzia kazi za vikundi vya vijana kufyatua matofali shilingi 81,500,000/=.
Ameongeza kuwa matumizi mengine kuwa ni usambazaji wa mashine uliyogharimu shilingi 30,000,000/=, uhakiki wa ubora wa mashine uliofanywa na wataalamu kutoka VETA shilingi 6,400,000/=, fedha za kununulia vifaa vya mafunzo katika kila halmashauri vilivyogharimu shilingi 130,400,000 na posho ya wakufunzi wa VETA ni shilingi 139,060,000/=.
Bi Suzan amewataka vijana kote nchini kutumia fursa hii kwa ajli ya maendeleo yao ikiwemo na kuondokana na tatizo la kukukosa ajira. Amayetaka mashirka mengine nchini kuiga mfano wa NHC ili kunusuru nguvu kazi hii kubwa.
Kwa upande mwingine, Meneja wa Huduma kwa Jamii wa NHC, Bw, Muungano Saguya amesema kuwa wadau zikiwemo Halmashauri, Maafisa Vijana wa Mikoa na wilaya kwa kushirkiiana na mamameneja wa mikoa wa NHC wathamini mradi huu kwa kufuatilia ufanisi wake ili mradi huo uwe endelevu.
Ameongeza kuwa mradiukiwa endelevuna kusaidia kupunguza tatizo la ajira kwa vijana, bajeti itaongezeka kwa mwaka wa fedhaujao ilikusaidia zaidi mradi huo kwa vijana.
Naye  Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa Mkoa wa Tabora, Bw. Erasto Chilambo amesema maafisa vijana wawaunganishe vijana katik a vikundi ili watumie fursa hii kujiendeleza na kuacha kubweteka na kulalamika kwa kukosa ajira.
Aliongeza kuwa vijana  wasiwe sehemu ya tatizo la ajira bali wawe  watatuzi wa changamoto inayowakabili ya kukosa ajira.
Kikao hiki ni kikao cha kuwakumbusha maafisa vijana majukumu yao  kuwasaidia kupata uzoefu toka kwa wenzao. Kimeandaliwa na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni