Jumamosi, 6 Juni 2015

Vijana watakiwa Kuwaepuka 

Wanasiasa Matapeli

Mpekuzi blog
VIJANA wilayani Tarime wametakiwa kuepuka baadhi ya wanasiasa wanaowatumia na kuwafanya kuwa daraja la kupandia ili kupata vyeo kwa maslahi yao binafsi.

Kauli hiyo ilitolewa hivi karibuni na Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Mfaume Ally Kizigo, wakati wa ziara yake ya kuhamasisha uhai wa chama wilayani Tarime.

Alisema kuna haja vijana kuepuka wanasiasa wanaowatumia kwa maslahi yao binafsi, huku wakiwaacha mitaani wakitaabika.

Aliwatahadharisha kabla ya kujiunga na chama chochote cha siasa wafanye upembuzi wa kina kuangalia kitakachowavusha badala ya kukimbilia vyama kwa ushabiki.

Alisema baadhi ya vijana wamekuwa wakikimbilia vyama vya upinzani kwa ushabiki, jambo ambalo huwarudisha nyuma kimaendeleo.

“Fanyeni utafiti kabla ya kujiunga na chama chochote cha siasa, ukijiunga na chama kwa kufuata mkumbo mwisho wa siku utajutia,” alisema Kizigo.
Mpekuzi blog

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni