Jumatatu, 23 Machi 2015

Umeskia hii ya mama kujifungua mara mbili ndani ya mwaka mmoja?

preee

Tuliwahi kuandika stori ya mwanamke kujifungua watoto mapacha ambao walipishana miezi miwili waliozaliwa katika moja ya hospitali huko Romania na kuonekana kugusa hisia za watu wengi.
sarah3Hii tena imetokea huko Uingereza baada ya mama mmoja kupata watoto wanne ikiwa ni matokeo ya kushika ujauzito mara mbili ndani ya mwaka mmoja.
Sarah Ward mwenye umri wa miaka 29 alipata mapacha watatu ikiwa ni mwezi mmoja tangu ajifungue mtoto wake wa kwanza wa kiume,
sarah
Mwanamke huyo alijifungua mapacha hao watatu ambao walizaliwa kabla ya muda huku mtoto wake wa kwanza akiwa tayari na miezi nane.
Sarah amesema anashukuru kupata watoto hao na amekua akitumia nepi zaidi ya 30 kwa siku kwa ajili ya kuwabadilisha watoto wake lakini haoni kama ni gharama kutokana na furaha aliyonayo.
sarah2Alisema alipata wakati mgumu wakati akijaribu kushika mimba ya mtoto wake wa kwanza na madaktari walipogundua ana mimba ya watoto mapacha watatu walimshauri kumtoa mmoja ili watakaosalia waweze kukua vizuri lakini alikataa na kutaka waache wote.
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia twitter instagram na facebook ukijiunga na mimi kwa kubonyeza >>> twitter Insta Facebook

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni